أخبار مصر

Al-Shurafaa Al-Hammadi: Nafasi ya Misri Kiarabu na Kikanda.‎

Hivi ndivyo historia ilivyotufundisha kupitia msimamo wa heshima wa ‎Misri, ambayo inajihusisha na Waarabu kwa mtazamo wa ndugu wa ‎kweli, inasimama nao katika masuala yao yote bila kudai gharama, ‎bila kujipendekeza, na bila maslahi ya kisiasa au ya kinyenzo. Badala ‎yake, inachota maadili yake ya Kiarabu kutoka kwenye historia ndefu ‎iliyothibitishwa kwa damu, mali, jasho na mapambano, pamoja na ‎kujitolea kwa wananchi wake kwa damu zao kwa ajili ya masuala ya ‎Kiarabu. Hayo ndiyo majaaliwa yake kisiasa, kijiografia, na kinchi; ‎Misri ni kama moyo katika mwili wa Kiarabu uliochoka na ‎unaogombana kwa mambo madogo madogo.‎

Wakati ninapotafakari historia ya taifa la Kiarabu katika nyakati zake ‎kuu za kuanguka, ninakuta kwamba Misri daima ndiyo nchi iliyobeba ‎mzigo mkubwa zaidi katika kulinda utambulisho wa Kiarabu na ‎kuhifadhi kilichobaki cha mshikamano wa mwili huu. Mwili ambao kwa ‎miongo mingi umekabiliwa na jaribio lililopangwa la kuusambaratisha, ‎lililolenga kuvunja taifa la kizalendo na kuwasha migogoro ya kiitikadi, ‎kidini, na kikabila kanda nzima igeuke kuwa uwanja wa wazi wa ‎vurugu, vita, na unyonyaji.‎

Nafasi Misri ya Kikanda
Mazungumzo kuhusu Misri si mazungumzo tu kuhusu mipaka ya ‎kijiografia, idadi ya watu, au nguvu za kijeshi; bali ni mazungumzo ‎kuhusu wazo la kistaarabu lililojikita katika historia yote ya ‎mwanadamu. Nchi hii iliyounda mojawapo ya staarabu za kale zaidi ‎duniani, imebaki kwa maelfu ya miaka ikiwa kituo cha utulivu wa ‎kanda. Wakati ilipokuwa ikidhoofika, taifa lote la Kiarabu lilikuwa ‎likiingia katika mizingo ya machafuko na kusambaratika, na wakati ‎ilipokuwa ikirejesha afya yake, kanda nzima ilirejesha sehemu ya ‎utulivu wake uliyopotea.‎

Kwa sababu hiyo, haikuwa ajabu kwa Misri kubeba katika historia ‎yake ya sasa mizigo inayozidi uwezo wake wa kiuchumi na kisiasa ‎wakati mwingine, kwa ajili ya kutetea masuala ya taifa la Kiarabu. ‎Kutoka Palestina hadi Algeria, na kutoka Yemen hadi Iraq, na kutoka ‎Lebanon hadi Libya, damu ya Mmisri ilikuwa ikishuhudiwa katika kila ‎vita vya kutetea usalama wa taifa la Kiarabu. Cairo ilibaki, japokuwa ‎na shinikizo na malengo yote iliyokabiliwa nayo, ikitengeneza kituo ‎kikuu cha utulivu kwa ajili ya utulivu wa mataifa ya kiarabu.‎

Misri imelipa gharama kubwa kwa ajili ya kushikilia nafasi yake ya ‎kitaifa. Imelipa kutoka kwenye uchumi wake, utulivu wake wa ndani, ‎na kutoka kwenye damu ya wananchi wake, kwa sababu ilikuwa ‎ikitambua kutokana na eneo lake la kijiografia na kihistoria kwamba ‎nchi yoyote ya Kiarabu kuingia katika vurugu kutaeneza athari zake ‎kwenye kanda nzima, na hazitabaki ndani ya mipaka yake pekee. ‎

Usalama wa taifa la Misri haukuwahi kutengwa na usalama wa taifa la ‎Kiarabu, na ukweli huu ulithibitishwa na jiografia kabla ya kuthibitishwa ‎na siasa.‎

Yeyote anayesoma ramani za migogoro katika kanda anatambua ‎kwamba kulenga Misri kuliwakilisha kulenga wazo la taifa kuu la ‎Kiarabu lenye uwezo wa kulinda mizania, na haikuwa kamwe kulenga ‎nchi moja pekee. Ndiyo maana Misri ilikabiliwa katika miongo kadhaa ‎na mawimbi ya mfululizo ya shinikizo, vita, njama, na majaribio ya ‎kidhoofisha; kwani kubaki kwake ikiwa imara kunamaanisha kubaki ‎kwa wazo la taifa la Kiarabu lenyewe likiwa hai na lenye uwezo wa ‎kustahimili.‎

Nguvu nyingi katika historia zilitambua kwamba kuiangusha Misri au ‎kuichosha kunafungua mlango hatari zaidi wa kuunda upya kanda ‎kulingana na ramani za usambaratishaji na vurugu. Ndiyo maana ‎tulishuhudia jinsi uwekezaji ulivyofanyika katika kuanzisha kundi la ‎Muslim Brotherhood katika miaka ya 1920 kutoka moyoni mwa Misri ili ‎kupiga mshikamano wa kitaifa na kusambaratisha muundo wa kijamii, ‎kueneza makundi ya msimamo mkali, kufadhili vurugu, na kupiga ‎taasisi za taifa

موضوعات ذات صلة

زر الذهاب إلى الأعلى